Lyrics
Abudiwa Bwana, tukuka Bwana,
Heshimika Bwana, tukuka milele,
Wewe ni Mungu hakuna kama wewe Bwana,
Unayotenda hakuna mwingine awezaye tenda,
Unarudishia watu miaka yao, waliopoteza
Unarudishia watu miaka yao, iliyoliwa na nzige
Ulimrudishia Ayubu miaka yote aliopoteza,
Mali yake watoto wote bwana ulirudisha,
Tena maradufu,
Bwana ulirudisha nami najua nitarudishiwa,
Miaka yangu nitarudishiwa,
Iliyoliwa na nzige nitarudisha,
Eeeiee miaka yangu,
Iliyoliwa na nzige,
Narudisha! narudisha!
Miaka yangu iliyoliwa na nzige,
Narudisha kwa jina la Yesu
Miaka yangu, iliyoliwa na nzige,
Narudisha! narudisha!
Miaka yangu iliyoliwa na nzige,
Narudisha kwa jina la Yesu
Narudisha! narudisha!
Narudisha kwa jina la Yesu
Nzige wamekula amani ya wengi,
Nzige wameharibu afya ya wengi mno,
Angalia imebaki mifupa mikavu,
Tazama imebakia mifupa mikavu,
Lakini kuna tumaini, Bwana atarudisha,
Amani itarudishwa, afya itarudishwa,
Biashara itarudishwa, furaha inarudishwa,
Waliopakwa tope, Bwana anasafisha,
Walioshushwa chini Bwana anainua,
Ata mti ukikatwa, utachipuka tena,
Waliopoteza maono yao jipe moyo,
Bwana anarudisha kwa jina la Yesu
Narudisha, narudisha,
Miaka yangu, iliyoliwa yote,
Narudisha kwa jina la Yesu,
Miaka yangu iliyoliwa na nzige,
Narudisha, narudisha,
Miaka yangu yote iliyoharibiwa
Narudisha kwa jina la Yesu
Vyote vyangu nilivyopoteza kwa nzige
Narudisha, narudisha
Mali yangu niliyopoteza mimi
Narudisha kwa jina la Yesu
Nasema yote niliyopoteza
Narudisha, narudisha
(narudisha, narudisha)
Narudisha kwa jina la Yesu